Jeremiah 13:1-6

Mkanda Wa Kitani

1Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ununue mkanda wa kitani, ujivike kiunoni mwako, lakini usiuache uguse maji.” 2Kwa hiyo nikanunua mkanda, kama Bwana alivyoniagiza, nikajivika kiunoni.

3 aNdipo neno la Bwana likanijia kwa mara ya pili: 4 b“Chukua mkanda ulionunua ambao umeuvaa kiunoni mwako, uende sasa Frati uufiche ndani ya ufa mdogo kwenye mwamba.” 5 cNdipo nikaenda na kuuficha ule mkanda huko Frati, kama Bwana alivyoniamuru.

6Baada ya siku nyingi Bwana akaniambia, “Nenda sasa Frati ukauchukue ule mkanda niliokuambia uufiche huko.”
Copyright information for SwhKC